School ConnectivityTanzania · East Africa
HomeAboutTeamNewsPublicationsGalleryContact Us
© School Connectivity
Back to all news

UDOM, UNICEF WALETA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KONDOA

25 June 2026kondoa - DodomaSchool Connectivity Team
UDOM, UNICEF WALETA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KONDOA

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Joseph, akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Amani Abeid Karume kuhusu fursa za kujifunza kidijitali, wakati wakikagua huduma ya mtandao imavyofanya kazi shuleni hapo na kusaidia wanafunzi kujifunza.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Joseph, akibadilishana mawazo na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kondoa, Bi. Sekela Mwasubila, kuhusu utekelezaji wa mradi wa Huduma ya Mtandao inayotolewa kwa shule 5 na ofisi 5 za Kata.

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kwa kushirikiana na UNICEF Tanzania, kimeanza kufungua ukurasa mpya wa maendeleo ya kidijitali katika Wilaya ya Kondoa, mkoani Dodoma, kupitia mradi wa kusambaza huduma ya intaneti kwa shule na jamii.

Katika ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo iliyofanyika leo Alhamisi, tarehe 19 Machi 2026, ikiongozwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Mdami, imeelezwa kuwa hatua kubwa tayari imefikiwa.

Msimamizi wa mradi huo, Dkt. Jabhera Matogoro, amesema vituo 10 tayari vimeunganishwa na huduma ya intaneti ya kasi ya 20Mbps, ikijumuisha shule tano za sekondari na Msingi, na vituo vitano vya jamii, hatua inayotarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika upatikanaji wa taarifa, ujinzaji na ufundishaji.

Ameeleza kuwa mradi huo unalenga kuwezesha walimu, wanafunzi na wananchi kwa ujumla kupata maarifa kwa urahisi kupitia mtandao, sambamba na kuchochea fursa za ajira, ubunifu wa kibiashara na maendeleo ya kijamii katika wilaya hiyo.

Soma zaidi Hapa 

Share this story:

You might also like

Continue reading more stories from our community

UDOM yaonesha nguvu ya tafiti na ubunifu wa kidijitali kuelekea Tanzania 2050
26 Jun 2026

UDOM yaonesha nguvu ya tafiti na ubunifu wa kidijitali kuelekea Tanzania 2050

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kupitia Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu (CIVE), kimezindua rasmi Wiki ya Utafiti na Ubunifu, ikianza kwa maonesho ya tafiti na bunifu za...

UDOM NA NMB WAHAMASISHA VIJANA KUTUMIA TECHNOLOGIA NA UBUNIFU KUJENGA MUSTAKABALI WAO
25 Jun 2026

UDOM NA NMB WAHAMASISHA VIJANA KUTUMIA TECHNOLOGIA NA UBUNIFU KUJENGA MUSTAKABALI WAO

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kupitia Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu kwa kushirikiana na Benki ya NMB, kimeandaa mhadhara wa wazi wa kitaaluma uliolenga kuwawezesha w...

UDOM and UNICEF Tanzania Joined to Support School Connectivity Programme
25 Jun 2026

UDOM and UNICEF Tanzania Joined to Support School Connectivity Programme

Towards Sustainable Schools and Communities InternetConnectivity Programme using TV Digital White Space On 14th March 2022, The University of Dodoma (UDOM) and UNICEF Tanzania has...